Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo Gari lakwamishwa pambano la Twaha kiduku na Dulla Mbabe
MichezoTangulizi

Gari lakwamishwa pambano la Twaha kiduku na Dulla Mbabe

Spread the love

 

PAMBANO la mchezo wa ngumi lililofahamika kwa jina la ‘Payback Night’ kati ya mabondia, Abdallah Pazi ‘Dulla Mbabe’ na Twaha Kassim ‘Twaha Kiduku’ limeahilishwa mara baada ya kukosekana kwa zawadi ya gari. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Pambano hilo awali lilipangwa kufanyika mwezi Julai, sasa litasogezwa mbele hadi tarehe 20 Agosti, 2021, baada ya kusaini mkataba wa makubaliano wa kucheza pambano hilo, tarehe 26 Mei, 2021.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, promota wa pambano hilo, Suleman Semunyu amesema pambano hilo hii leo tarehe 13 Juni 2021, huku akieleza kuwa kushindwa kupatikana kwa zawadi ya gari kwa sasa ndio kumepelekea tukio hilo kutofanyika kwenye tarehe hiyo.

Alisema kuwa “Ni kweli pambano limehailishwa, unakumbuka licha ya kuwalipa fedha kama sehemu ya mshahara kwenye pambano hilo, nikatoa nyongeza ili wapate gari kama zawadi kwa mshindi wa pambano hilo.

Aidha Semunyu aliongezea kuwa zawadi hiyo imepeleka mbele mpambano huo, kwa kuwa yupo kwenye mazungumzo na mtu ambaye alionesha nia ya kutoa gari hilo, lakini kwa muda uliobakia mpaka kufikia tarehe ya pambano hilo, haitawezekana.

“Nimeongea na mtu ambaye anaweza kuwa na nia ya kutoa gari, lakini kwa tarehe hiyo haitawezekana, bado tupo kwenye mazungumzo,” alisema promota huyo.

Promota huyo alisisitiza tarehe hiyo, mshindi kupata zawadi ya gari haitowezekana kama aliyeahidi wakati wa kuingia makubaliano hayo, lakini kama zawadi hiyo ikishindikana, pambano hilo litapigwa kwa kuwa haikuwa sehemu ya mapatano.

Pambano hilo litakuwa la pili kwa mabondia hao wenye uzito wa kati ‘Super Middle weight’ kufanyika ndani ya mwaka mmoja

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ampandisha cheo RPC wa Dar

Spread the loveMKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema...

error: Content is protected !!