Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Filamu ya Ndugai na wabunge yaendelea Dodoma
Habari za Siasa

Filamu ya Ndugai na wabunge yaendelea Dodoma

Job Ndugai,. Spika wa Bunge la Tanzania
Spread the love

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amesema  mbunge wa Ubungo Saed  Kubenea hajaitwa kwenye Kamati Ulinzi na Usalama ya Bunge kama mtuhumiwa wa kitu chochote, anaandika Hamis Mguta.

Ndugai amesema hayo leo bungeni akieleza kauli iliyotolewa na Mbunge wa  Arusha Mjini,  Godbless Lema akimshtumu Spika kuhusu sababu za kuwaita mbunge Kubenea na Zittp Kabwe kwenye kamati hiyo.

Amesema Bunge liliamua kuwa maombi yanayohusiana na usalama yaende kwenye kamati ya ulinzi baada ya Mbunge wa Nzega mjini, Husein Bashe (CCM),  kutoa ushauri huo.

“Hayo aliyoyasema Kubenea yanaweza kuisaidia kamati katika kazi zake, kwa hiyo kupelekwa Kubenea kwenye kamati ile hapelekwi kama mtuhumiwa wa kitu chochote.

“Anapelekwa ili anayoyasema barabarani ayaseme hapa kama mbunge,” amesema Ndugai.

Pamoja na kumshutumu Spika huyo,  akiwa mjini  Nairobi Lema alitaka Bunge kusimama baada ya Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema)Tundu Lissu kupigwa risasi akiwa Dodoma.

Ndugai amesema kuwa maombi hayo ya Lema kutaka Bunge lisimame baada ya Tundu Lissu kupigwa risasi si vizuri kwa kuwa hakuna kanuni zinazotaka hivyo isipokuwa  zinasema Mbunge akifariki ndiyo  litasimama kwa siku moja.

Awali Ndugai aliagiza Kubenea ajisalimishe popote alipo ili ahojiwa kwa madi ya kumuita Spika muongo.

Baada ya kutokea tukio baya la Lissu kupigwa risasi, Ndugai aliliambia Bunge idadi tofauti ya risasi alizopigwa huku  Kubea naye akitoa idadi nyingine isiyonana na ya kwake  kitendo ambacho Spika aliona kama mbunge huyo aliomuona yeye ni muongo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!