SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amesema mbunge wa Ubungo Saed Kubenea hajaitwa kwenye Kamati Ulinzi na Usalama ya Bunge kama mtuhumiwa wa kitu chochote, anaandika Hamis Mguta.
Ndugai amesema hayo leo bungeni akieleza kauli iliyotolewa na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema akimshtumu Spika kuhusu sababu za kuwaita mbunge Kubenea na Zittp Kabwe kwenye kamati hiyo.
Amesema Bunge liliamua kuwa maombi yanayohusiana na usalama yaende kwenye kamati ya ulinzi baada ya Mbunge wa Nzega mjini, Husein Bashe (CCM), kutoa ushauri huo.
“Hayo aliyoyasema Kubenea yanaweza kuisaidia kamati katika kazi zake, kwa hiyo kupelekwa Kubenea kwenye kamati ile hapelekwi kama mtuhumiwa wa kitu chochote.
“Anapelekwa ili anayoyasema barabarani ayaseme hapa kama mbunge,” amesema Ndugai.
Pamoja na kumshutumu Spika huyo, akiwa mjini Nairobi Lema alitaka Bunge kusimama baada ya Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema)Tundu Lissu kupigwa risasi akiwa Dodoma.
Ndugai amesema kuwa maombi hayo ya Lema kutaka Bunge lisimame baada ya Tundu Lissu kupigwa risasi si vizuri kwa kuwa hakuna kanuni zinazotaka hivyo isipokuwa zinasema Mbunge akifariki ndiyo litasimama kwa siku moja.
Awali Ndugai aliagiza Kubenea ajisalimishe popote alipo ili ahojiwa kwa madi ya kumuita Spika muongo.
Baada ya kutokea tukio baya la Lissu kupigwa risasi, Ndugai aliliambia Bunge idadi tofauti ya risasi alizopigwa huku Kubea naye akitoa idadi nyingine isiyonana na ya kwake kitendo ambacho Spika aliona kama mbunge huyo aliomuona yeye ni muongo.
Leave a comment