Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Filamu ya Ndugai na wabunge yaendelea Dodoma
Habari za Siasa

Filamu ya Ndugai na wabunge yaendelea Dodoma

Job Ndugai,. Spika wa Bunge la Tanzania
Spread the love

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amesema  mbunge wa Ubungo Saed  Kubenea hajaitwa kwenye Kamati Ulinzi na Usalama ya Bunge kama mtuhumiwa wa kitu chochote, anaandika Hamis Mguta.

Ndugai amesema hayo leo bungeni akieleza kauli iliyotolewa na Mbunge wa  Arusha Mjini,  Godbless Lema akimshtumu Spika kuhusu sababu za kuwaita mbunge Kubenea na Zittp Kabwe kwenye kamati hiyo.

Amesema Bunge liliamua kuwa maombi yanayohusiana na usalama yaende kwenye kamati ya ulinzi baada ya Mbunge wa Nzega mjini, Husein Bashe (CCM),  kutoa ushauri huo.

“Hayo aliyoyasema Kubenea yanaweza kuisaidia kamati katika kazi zake, kwa hiyo kupelekwa Kubenea kwenye kamati ile hapelekwi kama mtuhumiwa wa kitu chochote.

“Anapelekwa ili anayoyasema barabarani ayaseme hapa kama mbunge,” amesema Ndugai.

Pamoja na kumshutumu Spika huyo,  akiwa mjini  Nairobi Lema alitaka Bunge kusimama baada ya Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema)Tundu Lissu kupigwa risasi akiwa Dodoma.

Ndugai amesema kuwa maombi hayo ya Lema kutaka Bunge lisimame baada ya Tundu Lissu kupigwa risasi si vizuri kwa kuwa hakuna kanuni zinazotaka hivyo isipokuwa  zinasema Mbunge akifariki ndiyo  litasimama kwa siku moja.

Awali Ndugai aliagiza Kubenea ajisalimishe popote alipo ili ahojiwa kwa madi ya kumuita Spika muongo.

Baada ya kutokea tukio baya la Lissu kupigwa risasi, Ndugai aliliambia Bunge idadi tofauti ya risasi alizopigwa huku  Kubea naye akitoa idadi nyingine isiyonana na ya kwake  kitendo ambacho Spika aliona kama mbunge huyo aliomuona yeye ni muongo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!