Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Michezo FIFA ‘yamtupa jela’ Rais wa CAF miaka mitano
Michezo

FIFA ‘yamtupa jela’ Rais wa CAF miaka mitano

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (Caf), Ahmad Ahmad
Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Duniani (Fifa) limemfungia kujihusisha na shughuli za moita wa miguu kwa miaka mtano, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (Caf), Ahmad Ahmad baada ya kukutwa na hatia ya kukiuka sheria kadhaa za maadili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Ahmad ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Fifa, amedaiwa kukiuka sheria ya maadili inayohusisha jukumu lake la utiifu, kwa kutoa na kupokea zawadi hatua ambayo ni kinyume na wadhfa wake mbali na utumizi mbaya wa fedha.

Taarifa iliyotolewa na Fifa ilieleza kuwa, uchunguzi dhidi ya Rais huyo wa Caf ulianza mwaka 2017 hadi 2019 ulihusu masuala ya utawala wake katika shirikisho hilo pamoja na kuandaa na kufadhili safari ya kuhiji Makka, kuhusishwa kwake katika kashfa ya kampuni ya vifaa vya michezo ya Tactical Steel na shughuli nyengine.

Kabla ya hukumu hiyo kutolewa na Kamati ya Maadili ya Fifa, Ahmad ambaye anatokea nchini Madagascar alitangaza lengo lake kuwania muhula wa pili wakati uchaguzi wa Caf utakapofanyika mwezi Machi mwaka ujao.

Hilo huenda lisifanyike kwa sababu atalazimika kupita mtihani wa maadili ili kustahiki kusalia katika baraza la Fifa.

Uwezekano wa yeye kuchaguliwa kwa awamu ya pili utategemea iwapo atashinda kesi ya rufaa aliowasilisha katika mahakama ya kutatua mizozo ya michezo CAS, huku kesi hiyo akihakikisha kuwa inasikilizwa mapema ili kumruhusu kuthibitishwa kuwa mgombea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!