Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Fidia kwa wananchi: Serikali yaibana Tembo Nickel
Habari Mchanganyiko

Fidia kwa wananchi: Serikali yaibana Tembo Nickel

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imeagiza kampuni ya uchimbaji madini ya Tembo Nickel Corporation Ltd, kufanya upya tathimini ya fidia kwa wananchi wanaozunguka Mgodi wa Nickel wa Kabanga, ulioko Ngara mkoani Kagera. Anaripoti Mwandishi wetu, Dodoma…(endelea).

Maagizo hayo yametolewa leo Jumanne tarehe 27 Aprili 2021, na Naibu Waziri wa Madini, Prof. Shukrani Manya wakati akijibu swali la Mbunge wa Ngara (CCM), Ndaisaba Ruhoro, bungeni jijini Dodoma.

Katika swali lake, Ndaisaba aliihoji serikali akisema “kwa vile kuna tahimini ilifanyika hapo awali kwa ajili ya kutoa fidia kwa wananchi wanaozunguka mgodi huu, ambapo ni ya muda mrefu na ilipoteza uhalali. Je, serikali ina mpango gani kurudia kufanya tathmini ili wananchi waweze kupata fidia?”

Akijibu swali hilo, Prof. Manya amesema, tathimini iliyofanyika awali imepoteza uhalali kwa mujibu wa sheria, na kuiagiza Kampuni ya Tembo Nickel kufanya tathmini upya kwa ajili ya kulipa fidia, ili waanze mradi wao.

“Kuhusu tahimini, ni kweli ilifanyika miaka ya nyuma na kwa mujibu wa sheria ikipita miezi sita inaonekana haifai na hivyo inatakiwa kurudiwa, katika miradi yote ya uchimbaji mkubwa hakuna ulioanza bila kufanya tahimini na wananchi kulipwa malipo stahiki,” amesema Prof. Manya na kuongeza:

“Na tunaelekeza makampuni ya wachimbaji wafanye zoezi hilo kabla ya kuanza kuchimba. Katika hili, tutawaelekeza Tembo Nickel warudie kufanya tahimini ili wafanye fidia na hatimaye mradi uweze kuanza.”

Kampuni ya Tembo Nickel ilianzishwa baada ya Kampuni ya LZ Nickel ya nchini Uingereza kuingia ubia na Serikali ya Tanzania tarehe 19 Januari 2021, wa uchimbaji madini ya Nickel katika eneo la Kabanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!