Monday , 11 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Fedha za misaada kupungua kwa 38%, Serikali kukopa trilioni 12.29
Habari Mchanganyiko

Fedha za misaada kupungua kwa 38%, Serikali kukopa trilioni 12.29

Spread the love

FEDHA za misaada zinazotarajiwa kutolewa kwenye bajeti ya 2024/25, kwa ajili ya utekelezaji wa miradi na programu mbalimbali zimepungua kwa asilimia 38, ikilinganishwa na Sh. 1.11 trilioni, zilizoahidiwa 2023/24. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Akiwasilisha mwongozo wa maandalizi ya mpango na bajeti ya 2024/25, leo tarehe 6 Novemba 2023, bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba, amesema sababu za upungufu huo ni athari za ugonjwa wa UVIKO-19 na vita kati ya Urusi na Ukraine, vilivyoathiri uchumi wa nchi za Ulaya ambazo ni watoaji wakubwa wa misaada.

Dk. Mwigulu amesema, katika bajeti ya 2024/25, Serikali inatarajia kukopa Sh. 12.29 trilioni, kutoka vyanzo vya ndani na nje ya nchi, kwa ajili ya kuziba nakisi ya bajeti. Sh. 6.14 trilioni inatarajiwa kukopwa ndani ambapo Sh. 3.91 trilioni, inatarajiwa kulipa mikopoitakayoiva na Sh. 2.22 trilioni kwa ajili ya kuziba nakisi ya bajeti.

“Katika kipindi cha muda wa kati, Serikali itaendelea kukopa kutoka vyanzo vya ndani kwa kiwango kisichozidi asilimia 1.0 ya Pato la Taifa kwa mwaka ili kutoathiri upatikanaji wa mikopo kwa sekta binafsi,” amesema Dk. Mwigulu.

Kuhusu mikopo nje ya nchi, Dk. Mwigulu amesema Serikali inatarajia kukopa Sh. 6.15 trilioni, ikiwemo mikopo yenye masharti nafuu Sh. 3.60 trilioni na mikopo yenye masharti ya kibiashara Sh. 1.55 trilioni.

“Katika mwaka 2024/25, matumizi ya Serikali yanatarajiwa kuwa Sh. bilioni 47,424.9 (Sh. 47.42 trilioni). Kati ya kiasi hicho, deni la Serikali Sh. bilioni 12,101.2 (Sh. 12.10 trilioni), mishahara Sh. bilioni 11,774.8 (Sh. 11.77 trilioni)na uendeshaji wa shughuli za Serikali Sh. bilioni 8,223.8 (Sh. 8.22 trilioni). Aidha, matumizi kwa ajili ya programu na miradi ya maendeleo ni Sh. bilioni 15,325.1 (Sh. 15.32 trilioni)ikijumuisha ruzuku ya maendeleo,” amesema Dk. Mwigulu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Kesi ya mfanyakazi wa CRDB itaendelea J’tatu

Spread the love  MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam inatarajia...

Habari Mchanganyiko

Mawasiliano Dar – Bagamoyo yarejea

Spread the loveMAWASILIANO ya barabara ya Mkoa wa Pwani na Dar es...

Habari Mchanganyiko

Tanesco: Mvua chanzo kukatika umeme leo

Spread the loveShirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limedai kuwa hitilafu iliyojitokeza katika...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Zara tours yajivunia kupandisha wageni 228 Mlima Kilimanjaro

Spread the loveKampuni ya utalii ya Zara tours ya mjini Moshi mkoani...

error: Content is protected !!