Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Fatma Karume ataka mahakama ya kuchunguza vifo vyenye utata
Habari Mchanganyiko

Fatma Karume ataka mahakama ya kuchunguza vifo vyenye utata

Spread the love

 

ALIYEKUWA Rais wa Chama Cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Fatma Karume ameishauri uundwaji wa Mahakama maalum itakayochunguza vifo vinavyotokea katika mazingira yenye utata. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Fatma ametoa wito huo leo tarehe 11 Machi 2023 katika kongamano la kukusanya maoni ya wadau juu ya uboreshaji taasisi za haki jinai, lililoandaliwa na TLS na kufanyika jijini Dar es Salaam.

Mtetezi huyo wa haki za binadamu amesema kuwa, mahakama hiyo itasaidia Serikali kulinda maisha ya wananchi wake.

“Serikali na mfumo wa haki jinai haithamini maisha ya watu, tuseme Ulaya bila kujulikana sababu ya kifo changu kuna mahakama itaanza kushughulikia kujua nimefariki kutokana na sababu za asili au kuna kitu kingine,” amesema Fatma.

Fatma amesema “mahakama na Jaji Mkuu wana haki ya kuanzisha mahakama inayochunguxa vifo vya wanaokufa katika mazingira tatanishi. Watu wanakufa jela hakuna mahakama ya kuchunguza.”

Wakati huo huo, Fatma ameitaka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), kushughulikia kesi zilizokaa muda mrefu kwa sababu ya uchunguzi wake kutokamilika ili kutoa haki kwa watuhumiwa.

Ametoa wito huo baada ya Sheikh Said Ulatule, kufariki dunia kwa matatizo ya moyo, akiwa mahabusu alikokuwa anashikiliwa kwa tuhuma za ugaidi tangu 2016.

Katika hatua nyingine, Karume ameshauri Jeshi la Polisi kufuata sheria katika shughuli za ukamataji watuhumiwa mbalimbali ikiwemo kuwapa dhamana kwa wanaostahili na kuwapa haki ya kuwasiliana na ndugu zao.

Ameshauri Jeshi la Polisi kutoa taarifa kwa wakati pindi linapokamata watuhumiwa ili kuondoa wasiwasi kwamba wametekwa na wasiojulikana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!