Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Euro yanoga, vigogo waanguka
Michezo

Euro yanoga, vigogo waanguka

Spread the love

 

HATUA ya 16 bora ya michuano ya Euro imeanza mwisho wa juma lililopita ambapo mpaka sasa imeshapigwa jumla ya michezo minne, huku vigogo wa soka barani humo, Timu ya taifa ya Uholanzi na Ureno zikitupwa nje kwenye michuano hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Michezo miwili ya kwanza kwenye hatua hiyo ulipigwa siku ya Jumamosi, ambapo Denmark iliisukuma nje Wales kwa mabao 4-0, huku Italia ikitinga hatua ya robo fainali kwa ushindi wa mabao 2-1, dhidi ya Austria.

Hatua hiyo pia iliendelea tena siku ya jana kwa kupigwa michezo miwili ambayo ilishuhudia vigogo wakisukumwa nje.

Jamhuri ya Czech iliituoa nje, timu ya Taifa ya Uholazi maa baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-0, huku bingwa mtetezi Ureno wakiondoshwa mara baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0, dhidi ya Ubeligiji.

Wachezaji wa Ubelgiji wakishangilia ushindi dhidi ya Ureno

Ureno inatoka kwenye michuano hiyo mara baada ya kuingia kwenye 16 kwa mlango wa nyuma (Best Looser), kwenye kundi F, mbele ya Ufaransa na Ujerumani.

Nahodha wa kikosi hiko Cristiano Ronaldo anaondoka kwenye michuano hiyo, huku akiwa kinara kwenye ufungaji mara baada ya kupachika mabao 5, katika michezo minne aliyocheza kwenye michuano hiyo.

Michuano hiyo pia itaendelea tena hii leo kwenye hatua hiyo ya 16 bora, kwa kupigwa michezo miwili, ambapo Crotia itavaana na Hispania huku mabingwa wa Dunia, timu ya Taifa ya Ufaransa itamenyana na Uswizi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!