Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Eto’o kuzindua uwanja wa soka Tanzania
Michezo

Eto’o kuzindua uwanja wa soka Tanzania

Spread the love

NAHODHA wa zamani wa timu ya taifa ya Cameroon, Samuel Eto’o anataraajia kuja nchini Tanzania tarehe 10 Oktoba mwaka huu, kuzindua ujenzi wa kiwanja cha mchezo wa mpira wa miguu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Uwanja huo ambao utakuwa unachezewa mpira wa miguu kwa wachezaji watano (Five a side) utajengwa katika eneo la Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Etoo ambae atakuja chini ya udhamini wa Tanzania Breweries Limited (TBL) kupitia bia ya Catle Lager ambao wanaendesha kampeni maalumu ya inayofahamika kama (Castle Africa 5s).

Mmoja wa wakilishi kutoka TBL alisema kuwa wameamua kuendeleza mchezo huu hapa Tanzania kwa kujenga kiwanja maeneo ya Oysterbay ambacho kitatambulika kama (Castle Africa Five football pitch).

“Hichi kiwanja kwa kweli kitaweza kusaidia kukuza mpira huu, na sisi tunawaambia watanzania hili jambo zuri sana kwa sababu sasa hivi mpira ni sehemu inayotumika kuingiza mapato” alisema mwakilishi huyo.

Eto’o ambaye ameshawahi kutua katika ardhi ya Tanzania zaidi ya mara mbili akiwa na timu ya taifa ya Cameroon walipokuja kucheza na timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ katika michuano tofauti ya kimataifa ambayo ipo katika kalenda ya Shirikisho la mpira wa miguu Duniani FIFA.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!