LIGI Kuu England inaendelea tena leo kwa kupigwa michezo mitano ambapo Manchester United itashuka dimbani kuikabili Sheffield United kwenye dimba la Old Traford. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Michezo mingine kwenye ligi hiyo itaikutanisha Liverpool ambao wataikalibisha Crystal Palace, Norwich City dhidi ya Everton, Wolverhampton wanderers na Bournemouth na Newcastle United wataikabili Astorn villa.
Ligi hiyo ambayo ilisimama kwa miezi mitatu kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Covid-19, imesalia michezo nane kumalizika kwa msimu huu.
Mpaka sasa liverpool ndio vinara kwenye msimamo wa ligi akiwa na pointi 83, huku akifuatiwa na Manchester City mwenye pointi 63, Leicester city pointi 55 na nafasi ya nne akiwa Chelsea akiwa na pointi 51, na nafasi ya mwisho ikishwa na Norwich yenye alama 21, huku klabu za Astornvilla, Bournemouth na West Ham United zikipambana kutoshuka daraja.
Leave a comment