Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Elimu yapunguza ukeketaji Simanjiro
Habari Mchanganyiko

Elimu yapunguza ukeketaji Simanjiro

Spread the love

KUTOKANA na juhudi zinazofanywa na wanaharakati kwa kupinga unyanyasaji na utatili kwa watoto wa kike na akina mama na kutoa elimu juu ya madhara ya ukeketaji,  juhudi hizo zimepelekea Ukeketaji kupungua katika Wilaya ya Simanjiro. Anaripoti Dany Tibason, Dodoma … (endelea).

Hayo yalielezwa  Jijini hapa na Mwanaharakati wa kupinga ukeketaji kutoka Mtandao wa kupinga madhara ya ukeketaji nchini (Nafgem) Nagalali Therritho.

Therritho alitoa maelezo hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika banda la Nafgem, katika maonesho ya wiki ya AZAKI 2018 inayofanyika kitaifa Jijini Dodoma.

Kwa mujibu wa Mwanaharakati huyo,alisema awali katika eneo la Simanjiro ukeketaji ulikuwa upo juu lakini mara baada ya kufika Nafgem na kutoa elimu ukeketaji umepungua.

“Sina takwimu lakini kwa sasa ukeketaji umepungua sababu ni elimu tuliyoenda kutoa katika eneo la Simanjiro,” alisema.

Alisema yeye ni mzaliwa wa Simanjiro na alikwepa kukeketwa wakati akiwa mwanafunzi na alisaidiwa na Nafgem.

“Mimi nimesomeshwa na Shirika hili,nilitaka kukeketwa lakini wakanisaidia,sasa hivi natoa elimu na nilienda kutoa elimu, Simanjiro, japokuwa wazazi walinikataa lakini sasa hivi wamenikubali mara baada ya kuona nina kazi,” alisema.

Alisema awali mbinu iliyokuwa ikitumika kukeketa ilikuwa ni kuwakeketa watoto wakiwa wachanga.

“Mara baada ya kuona tunawabana sana wakiwa wanasoma,walikuja na mbinu nyingine ya kuwakeketa watoto wachanga,tulipambana na hili limeisha kwa sasa,” alisema.

Alisema changamoto kubwa wanayokutana nayo ni ukosefu wa maji katika eneo la Simanjiro hivyo watoto wengi kupata ugonjwa wa Lawalawa ambao husababisha uke kuwasha.

“Huu ugonjwa mtoto anawashwa kwenye uke,anakuwa anajikuna hivyo mzazi anaambiwa dawa pekee ni kukeketwa jambo ambalo sio kweli,tumetoa elimu kuhusiana na hili na wametuelewa,” alisema.

Alisema mara baada ya kuwaokoa watoto ambao walitaka kukeketwa wamewapeleka shule pamoja na katika Vyuo vya Ufundi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!