Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Dulla Mbabe ajiweka kando na masubwi
Michezo

Dulla Mbabe ajiweka kando na masubwi

Abdallah Pazi ‘Dulla Mbabe’
Spread the love

 

BONDIA wa Tanzania, Abdallah Pazi maarufu kama ‘Dulla Mbabe’ ametangaza rasmi kujiweka kando na masuala ya masubwi mpaka mwakani hii. Anaripoti Damas Ndelema, TUDARCo … (endelea).

Dulla Mbabe amefikia uamuzi huo ikiwa ni siku chache zimepita baada ya kupoteza pambano lake juzi Jumamosi dhidi ya Mjongo Tshimanga Katompa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Bondia huyo rekodi yake imechafuliwa kwa siku za karibuni katika mapambano aliyopigana baada ya kupoteza yote ambapo pambano la mwisho alitwangwa na Mtanzania mwenzi Twaha Kiduku.

“Mwakani ndio nafikiria kurudi ulingoni, ala kwa sasa wacha nipumzike kwanza nitulize akili nijipange upya… ili niwe na ujio mpya nitakaporejea tena ulingoni” amesema.

Katika pambano lake dhidi ya Mkongo huyo, Dula Mababe alipoteza kwa pointi za majaji wote watatu.

Kufuatia hali hiyo baadhi ya mabondia wakubwa hapa nchini kama Hassani Mwakinyo na Twaha Kiduku wamempa salamu za pole bondia mwenzao na kumtia hamasa.

“Asikate tamaa kwani hawezi kuwa bigwa bila kupoteza, lakini mchezo una matokeo matatu kushinda, kupoteza na kutoka sare…. hivyo tupo pamoja naye pia asikate tama,” wamesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!