DUBAI imefuta ushuru wa asilimia 30 kwenye bidhaa za pombe ili kuvutia zaidi watalii watembelee jiji hilo.
Pia imepanga kuacha kutoza leseni za pombe binafsi ili mtu yeyote anayenuia kunywa pia abebe kama anahitaji kufanya hivyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Dubai imekuwa ikilegeza sheria mbalimbali ikiwamo kuruhusu uuzaji wa pombe mchana wakati wa mfungo wa Ramadhani na kuidhinisha mauzo ya pombe majumbani wakati wa janga la Corona.
Hatua hii ya sasa inaelezwa kuwa ni jaribio la kulifanya jiji kuvutia wageni zaidi licha ya ushindani kutoka kwa majirani.
Kampuni mbili zinazosambaza pombe huko Dubai, Maritime na Mercantile International (MMI), na African & Eastern, zilisema zitaakisi kupunguzwa kwa ushuru kwa watumiaji.
Kanuni hizi zilizosasishwa hivi majuzi ni muhimu kuendelea kuhakikisha ununuzi na unywaji salama na unaowajibika wa vileo huko Dubai na UAE.
Haijabainika iwapo hatua hiyo iliyoanza kutekelezwa jana tarehe 1 Januari, 2023 itakuwa ya kudumu.
Dubai kihistoria imeweza kuvutia watalii zaidi na wafanyakazi matajiri wa kigeni kuliko majirani zake, kwa sehemu kwa sababu ya uvumilivu wake wa maisha ya huria zaidi.
Lakini sasa inakabiliwa na ushindani unaoongezeka kutoka kwa wapinzani wanaoendeleza sekta zao za hoteli, burudani na fedha.
Wasio Waislamu nchini Dubai lazima wawe na umri wa angalau miaka 21 ili kunywa pombe, na kubeba leseni ya pombe – kadi ya plastiki inayotolewa na polisi.
Ingawa baa na vilabu vya usiku ni nadra sana kuviomba vibali hivyo wale wanaokunywa pombe bila vibali wanaweza kutozwa faini au kukamatwa.
Leave a comment