Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa DR Congo yashtukia njama ya kuitikisa serikali
Kimataifa

DR Congo yashtukia njama ya kuitikisa serikali

Spread the love

 

WACHUNGUZI kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamesema wanao ushahidi wa kutosha unaoonyesha hatua kwa hatua namna maadui wanavyotaka kuiyumbisha nchi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Katika taarifa iliyosomwa kwenye televisheni ya taifa jana tarehe 8 Februari, 2022 na Msemaji wa Rais Felix Tshisekedi, Tharcisse Mwema amesema jaribio hilo linalolenga kuvuruga taasisi za kidemokrasia halitavumiliwa.

Taarifa hiyo imetolewa siku chache baada ya François Beya ambaye ni mshauri maalum wa usalama wa Rais Tshisekedi kukatamwa tarehe 5 Februari mwaka huu.

Tukio hilo lilitokea wakati rais huyo alipokuwa akihudhuria mkutano wa kilele wa Umoja wa Afrika katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa.

Kukamatwa kwa kigogo huyo kulizua maandamano, huku wanachama wa chama cha rais wakiingia mitaani.

Aidha, Msemaji huyo wa rais amesema uchunguzi unaendelea na hali imedhibitiwa.

Pamoja na mambo mengine imeelezwa kuwa ukimywa wa serikali na ofisi ya rais tangu kisa hicho cha Jumamosi kutokea, kimechochea tetesi za ukosefu wa utulivu nchini.

Hadi sasa Beya na hata mawakili wake hawajatoa taarifa yoyote kwa umma kuhusiana na kukamatwa kwake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!