MKURUGENZI mpya wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP), Sylvester Mwakitalu, ametangaza neema kwa mahabusu, wafungwa na watuhumiwa wengine wanaokabiliwa na mashtaka ya jinai mahakamani. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).
Katika mahojiano maalum na MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV, ofisini kwake, jijini Dar es Salaam jana, Alhamisi, tarehe 17 Juni 2021, Mwakitalu alisema, jukumu lake, ni kupeleka mahakamni ushahidi wa kuthibitisha makosa yaliyotendwa, siyo kubambikiza watu mashtaka ambayo mwisho wa siku, hayawezi kuthibitika mahakamani.
Amesema, “niwahakikishie Watanzania hii kazi tutaifanya kwa weledi, kwa uaminifu, haki na tutafanya kile ambacho tunapaswa kukifanya kwa mujibu wa katiba na sheria zetu.”
Nini amezungumza kuhusu, mageuzi makubwa ya kushuka mamlaka mikoani na wilayani, operesheni maalum na mengine mengi, ikiwemo kufuta kesi, soma Gazeti la Raia Mwema la leo Ijumaa, tarehe 18 Juni 2021. Pia, tembelea MwanaHALISI TV kupata mahojiano yote.
Leave a comment