Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko DPP aweka pingamizi kesi ya ‘watu wasiojulikana’
Habari Mchanganyiko

DPP aweka pingamizi kesi ya ‘watu wasiojulikana’

Spread the love

 

MKURUGENZI wa Mashtaka nchini (DPP), ameweka pingamizi dhidi ya kesi ya jinai iliyofunguliwa na Mwandishi wa Habari Luqman Maloto, kuhoji ukimya wa mamlaka za Serikali dhidi ya matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu, akidai kwamba Mahakama Kuu, Masjala Kuu, jijini Dar es Salaam, haina mamlaka ya kuisikiliza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Pingamizi hilo limewekwa mahakamani hapo leo tarehe 8 Februari 2023 na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi, wakati kesi hiyo Na.5/2023 ilipoletwa kwa ajili ya kutajwa mbele ya Jaji John Nkwabi.

Baada ya Wakili Nkwabi kuwasilisha taarifa ya kusudio la kuweka mapingamizi hayo, Jaji Nkwabi ameahirisha kesi hiyo hadi tarehe 22 Februari mwaka huu, ambapo yataanza kusikilizwa kabla ya kesi hiyo kutajwa.

Pingamizi hilo ya DPP yamebeba hoja sita, ikiwemo mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kusikiliza maombi hayo, hati ya kiapo cha maombi hayo kuwa na dosari za kisheria ziszioweza kutibika na maombi hayo kutokuwa na uwezo kisheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!