Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko DPP awafutia kesi uhujumi uchumi Wachina 6
Habari Mchanganyiko

DPP awafutia kesi uhujumi uchumi Wachina 6

Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu
Spread the love

 

MKURUGENZI wa Mashtaka nchini (DPP), Sylvester Mwakitalu, amewafutia shtaka la uhujumu uchumi raia sita wa China, wanaofanya kazi katika Kampuni ya Meli ya Sinota Shipping Company. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Ijumaa, tarehe 18 Juni 2021 na Wakili wa Serikali, Kija Luzuguna, wakati kesi ya uhujumu uchumi Na. 57/2020, ilipoitwa kwa ajili ya kutajwa, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Rais hao wa China, waliokuwa wanashtakiwa kwa kesi hiyo mahakamani hapo ni, Chengfa Yang (49), Shu Nan (50), Jin Erhao (35), Gu Jugen (57), Ren Yuangqing (55) na Chen Shinguang (45).

Akizungumza mahakamani hapo, Wakili Luzuguna amedai kuwa, DPP hana nia ya kuendelea na shauri hilo.

Baada ya taarifa hiyo, Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo, aliifuta kesi hiyo na kuwaacha huru raia hao wa China.

Katika kesi hiyo, Wachina hao walikuwa wanakabiliwa na mashtaka matatu, ambayo ni kusimamia genge la uhalifu uliopelekea kupatikana kwa ndege mmoja aina ya tausi, mwenye thamani ya Sh. 1,150,000. Walilodaiwa kufanya tarehe 11 Agosti 2020.

Shtaka la pili ni kukutwa na nyara ya Serikali, kinyume cha sheria, huku la tatu likiwa ni kukutwa na tausi huyo huku wakijua kummiliki ndege huyo ni kinyume cha sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!