Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko DPP awafungulia kesi ya uhujumu uchumi askari watatu
Habari Mchanganyiko

DPP awafungulia kesi ya uhujumu uchumi askari watatu

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania (DPP), Biswalo Mganga
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania, imekusudia kuwafungulia mashtaka ya uhujumu uchumu askari watatu wa Wanyama Pori kwenye Pori tengefu la Kilombero, Mkoa wa Morogoro. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).   

Katika taarifa iliyotolewa kwa umma na Mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania (DPP), Biswalo Mganga jana Ijumaa tarehe 15 Januri 2021, imeeleza mbali na askari, watashitakiwa pamoja na watu wengine zaidi ya watano kwa makosa ya uvamizi wa eneo tengefu la pori hilo na kutishia  kutoweka kwa wanyamapori na kuharibu pori hilo linalochangia asilimia 65 ya maji ya mto Rufiji.

Askari hao watashitakiwa kwa kujihusisha na uhalifu kinyume na sheria ya kuzuia makosa ya uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya ofisi na kushawishi kupewa rushwa.

Askari hao ni Elisante Ako, Vicent Mkuki na Joshua Magesa.

Watuhumiwa wengine ni; wakulima waliovamia eneo hilo ambao ni Samwel Tango, Jobu Mheni, Pascal Mtwango, Bosco Kindanda, Ernest Ngonyani, John Heguye, Fred Mjoge, Devotha Ngonyanina na Mwenyekiti wa Kijiji cha Ipugasa, Mkasiwa Shabani na Paulo Mwambope.

Taarifa ya DPP inaalelza, ofisi yake imepokea jalada la upelelezi wa shauri hilo wa tangu tarehe 2 Desemba 2020 hadi tarehe 13 Januari 2021, ambapo askari hao hawakuchukua hatua kwa wavamizi hao ikiwa wao ndio waliokuwa doria kwenye eneo hilo.

Askari hao wanadaiwa kutowajibika  pamoja na kutengeneza mazingira ya kupokea rushwa kutoka kwa watu wanaodaiwa kuvamia eneo hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

error: Content is protected !!