Friday , 2 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa DPP aikabidhi BoT fedha, madini yaliyotaifishwa
Habari za Siasa

DPP aikabidhi BoT fedha, madini yaliyotaifishwa

Biswalo Mganga, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania (DPP)
Spread the love

BISWALO Mganga, Mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania (DPP) ameikabidhi Benki Kuu ya Tanzania (BoT) madini ya dhahabu, vito mbalimbali na fedha za kigeni, zilizotaifishwa kutoka kwa wahujumu uchumi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Leo tarehe 29 Juni 2019 Jijini Dar es Salaam, Mganga amemkabidhi Dotto James, Katibu Mkuu wa Hazina madini ya dhahabu yenye uzito wa zaidi ya Kg. 18 yenye thamani ya kiasi cha Dola laki 6.6 na vito vya thamani vyenye uzito wa Kg 2849.45, yenye thamani ya dola laki 3.

Mganga amemkabidhi James madini hayo mbele ya Dk. Phillip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango, Balozi Augustine Mahiga, Waziri wa Katiba na Sheria na Dotto Biteko, Waziri wa Madini,

Akizungumza baada ya makabidhiano hayo, Biteko ameitaka BoT kuzitunza dhahabu hizo.

“BoT muitunze dhahabu hii, kwa kuwa ni wa kweli waaminifu hatuhitaji zile zama za dhahabu bandia zirudiwe,” ameagiza Biteko.

Balozi Mahiga ametoa wito kwa vyombo vya dola pamoja na mahakama kumaliza changamoto ya utoroshaji madini ili rasilimali hizo zisaidie Watanzania.

“Lakini nataka nipongeze wafanyakazi walioko chini yangu ofisi ya DPP na mahakama, muendelee hivyo. Hii ni asilimia ndogo tu ya uhalifu unaoendelea kuhusiana na utoroshaji wa madini, tuongeze jitihada hali na nguvu katika kulinda rasilimali za nchi yetu,” amesema Balozi Mahiga.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Mganga amesema madini hayo yalikamatwa na vyombo vya dola yakiwa njiani kutoroshwa kwenda nje ya nchi.

“Katibu mkuu wizara ya fedha hizi ni Kg 18.354 za dhahabu zenye thamani ya dola laki 6.6 nilizosema, walitunza wakati wanatorosha, naomba katibu mkuu nikukabidhi,” amesema Mganga.

James amesema BoT itahifadhi dhahabu hizo hadi pale serikali itakapotoa maelekezo ya matumizi ya madini hayo.

“Nilichokuwa natekeleza kama katibu mkuu hazina ni jukumu langu kuhakikisha nasimamia mali zote za serikali, hiki kilichokuwa kinafanyika hapa ni mali zilizopatikana kupitia ofisi ya DPP, “ amesema James na kuongeza.

“Mali hizi tulizozipata hapa ikiwemo madini na fedha taslimu ni zilizotaifishwa kupitia Ofisi ya DPP, mali zinapotaifishwa zinarudi mikononi mwa serikali vyovyote iwavyo kama kuna kesi inaendelea na serikali ikashinda mali hizi zinakuwa ni za serikali.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!