Tuesday , 26 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Dotto Biteko afunguka uteuzi wa Rais Samia
Habari za Siasa

Dotto Biteko afunguka uteuzi wa Rais Samia

Spread the love

NAIBU Waziri Mkuu, Dotto Biteko, amesema Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa jukumu kubwa baada ya kumteua kushika wadhifa huo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Biteko ametoa kauli hiyo leo tarehe 6 Septemba 2023, jijini Dodoma, akizungumza katika mkutano wa maafisa ustawi wa jamii.

“Nimshukuru Rais Samia kwa kuniona miongoni mwa wengi kuwa nina uwezo wa kumsaidia nafasi hii, katika hatua ya mwanzoni si busara sana kuahidi mbingu lakini nataka niseme kwa moyo wa dhati nimeupokea uteuzi huu nikiwa na wajibu mkubwa mbele yangu, nikiwa na kazi kubwa mbele yangu,” amesema Biteko na kuongeza:

“Lakini kwa sababu Rais amenipa kazi hii, jambo ambalo namuomba Mungu ni kunipa bega la kubeba majukumu haya. Lakini katika jambo ambalo sitafanya kosa ni kukosea ili aliyenitumia asije akakwazika kesho akateua mwingine.”

Biteko aliyekuwa Waziri wa Madini, aliteuliwa na Rais Samia kuwa Naibu Waziri Mkuu, mwishoni mwa Agosti mwaka huu, pamoja na kuhamishiwa katika Wizara ya Nishati.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za Siasa

Kamugisha aanika utekelezaji mpango kazi 2022/23

Spread the loveMWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama Cha ACT-Wazalendo Mkoa...

Habari za Siasa

Vijana ACT-Wazalendo wakabidhiwa kivumbi kulinda kura uchaguzi 2024,2025

Spread the loveNGOME ya Vijana ya Chama cha  ACT-Wazalendo, imetakiwa kuwanoa wafuasi...

error: Content is protected !!