Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Dodoma waomba muda vitambulisho vya Taifa
Habari Mchanganyiko

Dodoma waomba muda vitambulisho vya Taifa

Spread the love

WAKAZI wa kata ya Kizota Manispaa ya Dodoma ambao kwa hivi sasa wapo kwenye zoezi la uandikishaji wa vitambulisho vya taifa, wameomba muda uongezwe ili kuondokana na changamoto ya kukaa muda mrefu kwenye vituo vya kuandikishia. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Wakizungumza wakati wa kuandikisha vitambulisho hivyo katika kata ya Kizota baadhi ya wakazi hao wamesema, kutokana na muitikio wa wananchi kuwa wengi tunaomba muda uliowekwa wa siku tatu uongezwa kwa kuwa ni mdogo.

Fred Kombe mkazi wa Kizota amesema kuwa kutokana na wingi wa wananchi wanaojitokeza kwenye vituo, tunaomba serikali kuangalia kwa umakini ili zoezi hilo liweza kuwafikia watu wote.

“Kutokana na umuhimu wa zoezi hili tunaomba serikali iangalie kwa makini hii ni kutokana na mwitikio mkubwa uliotolewa kwa wanchi wa kuona faida ya kuwa na kitambulisho cha uraia,” amesema.

Naye Nazaeli Julias amesema kuwa muda ambao umepangwa kuna hatari wa wakazi wengi kuikosa fursa ya kujiandikisha kwa wakati, hivyo ni vizuri serikali ikatafakari ili kuwepo kwa muda wa kutosha.

Kwa upande wake, Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) mkoa wa Dodoma, Khalid Mrisho amesema kuwa licha ya kukabiliana na watu wengi lakini wamefanikiwa kuweka mashine nyingi ili kuhakikisha kila mmoja kuweza kuandikishwa.

“Pamoja na wingi wa watu wanaofika kujiandikisha bado mashine hizo zina uwezo wa kukabiliana na changamoto kutokana na kuwa na asilimia kubwa ya kuwaandikisha watu wote wanaofika kwenye vituo vya uandikishaji,” amesema.

Naye Mkuu wa Uhamiaji mkoa wa Dodoma, Peter Kundy ambaye ofisi yake inashirikiana bega kwa bega na NIDA, amesema kuwa lengo ni kuhakikisha vitambulisho vinapatikana kwa wananchi wote na kuhakikisha wageni wenye sifa waweze kupata na kutojipenyeza watu wasio na sifa kuweza kupata.

Amesema zoezi hilo la uandikishaji wa vitambulisho vya taifa linaendelea katika kata mbalimbali za mkoa mbali hapa Dodoma ili kuwawezesha wananchi wake kupata vitambulisho hivyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!