Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Tulia: Asilimia 60 ya fedha za bajeti zimetolewa
Habari Mchanganyiko

Dk. Tulia: Asilimia 60 ya fedha za bajeti zimetolewa

Spread the love

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Dk. Tulia Ackson, amesema Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imetoa asilimia 60.5 ya fedha zilizotengwa katika bajeti ya 2021/2022, katika kipindi cha muda mfupi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Spika Tulia amesema hayo leo Jumamosi, tarehe 19 Machi 2022, akifungua kongamano la tathmini ya mwaka mmoja wa Rais Samia madarakani, lililofanyika kwenye Chuo Kikuu cha Dodoma.

“Kwa ujumla ukifanya tathimini ya hizi takwimu unapata wastani wa asilimia 60.5 kutoka Julai 2021 mpaka kufikia Januari 2022. Hizi ni asilimia kubwa sana ukilinganisha na vipindi vingine,” amesema Spika Tulia.

Spika Tulia amesema, Wizara ya Afya imepokea asilimia 62.32, wakati Wizara ya Maji ikipokea asilimia 76.51 huku Wizara ya Maliasili na Utalii ikipokea asilimia 58.08. Wizara ya Ujenzi (60.69), Uchukuzi (23.32), Wizara ya Elimu (69.31) na Ofisi ya Rais-TAMISEMI (36.46).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!