Saturday , 3 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Tulia ang’oa hotuba ya Sugu bungeni
Habari za Siasa

Dk. Tulia ang’oa hotuba ya Sugu bungeni

Joseph Mbilinyi 'Sugu' Mbunge wa Mbeya Mjini
Spread the love

SPIKA wa Bunge, Dk.Tulia Ackson ameamuru kuondolewa kwenye kumbukumbu za bunge Hotuba ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2019/20 baada ya kuvutana na waziri kivuli wa wizara hiyo, Joseph Mbilinyi (Sugu), Mbunge wa Mbeya Mjini. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Hatua hiyo imefikiwa baada ya Sugu kulalamika na kugoma kusoma hotuba aliyowekewa mezani kwa madai kuwa, hotuba hiyo siyo ile iliyoandaliwa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Hotuba hiyo ambayo ilitakiwa kuwasilishwa na Sugu, aliigomea licha ya Dk.Tulia kutaka aendelee kusoma hiyo hiyo.

Katika msuguano huo Sugu amesema, hawezi kusoma hotuba hiyo kwa kuwa, alichopaswa kusoma ndani ya ukumbi wa bunge si maoni yake bali ya upinzani. Amesisitiza kuwa “siwezi kulishwa maneno.”

Sugu amelalamika kuwa, imekuwa kawaida ya kiti cha spika kutaka kuizuia hotuba ya yake ili asiweze kuisoma akidai ni dalili za uoga wa serikali.

Kutokana na hali hiyo, Dk. Akson alisema kitendo cha Sugu kutowasilisha hotuba yake bungeni, hakitakuwa katika kumbukumbu za taarifa za Bunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!