Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Tulia amdhibiti Mbunge wa CCM
Habari za Siasa

Dk. Tulia amdhibiti Mbunge wa CCM

Dk. Tulia Ackson, Naibu Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
Spread the love

TULIA Ackson, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemtaka Rashidi Shangazi, Mbunge wa Mlalo, mkoani Tanga kufuta kauli yake juu ya Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, baada ya kuiita kambi hiyo kuwa ni kambi rasmi ya upotoshaji, anaandika Hellen Sisya.

Tukio hilo limetokea leo bungeni mjini Dodoma katika kikao cha mwisho cha bunge ambapo mbunge huyo alikuwa akichangia mjadala unaohusu miswada mitatu ya ulinzi wa rasilimali na maliasili za nchi.

Kauli ya Mbunge huyo ilimnyanyua kitini Abdallah Mtolea, Mbunge wa Temeke (CUF) ambaye aliomba utaratibu kwa mujibu wa kanuni za bunge akitaka Shangazi afute maneno yake kwani ni kinyume cha kanuni hizo.

Naibu Spika alikubaliana na hoja ya Mtolea na kumtaka mbunge huyo kuheshimu kanuni za bunge na kuondoa maneno ya kuudhi aliyoyasema na badala yake kutumia maneno sahihi yanayotakiwa.

“Mheshimiwa Rashid Shangazi, naomba ufute maneno uliyoyasema kwasababu ni kinyume cha kanuni za bunge. Weka maneno yanayotakiwa kuwepo,” alisema Dk. Tulia.

Agizo hilo lilitekelezwa na Mbunge huyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!