Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Samia aagiza milioni 960 za uhuru kujenga mabweni
Habari Mchanganyiko

Dk. Samia aagiza milioni 960 za uhuru kujenga mabweni

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), George Simbachawene
Spread the love

 

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameagiza fedha kiasi cha Sh. 960 milioni, zilizotengwa kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 61 ya uhuru wa Tanzania Bara yaliyotarajiwa kufanyika kitaifa 2022, kwenda kujenga mabweni katika shule nane za msingi za watu wenye mahitaji maalum. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Uamuzi huo umetangazwa leo Jumatatu, tarehe 5 Desemba 2022 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), George Simbachawene, akizungumza na wanahabari kuhusu maandalizi ya maazimisho hayo, jijini Dodoma.

Simbachawene amesema, Rais Samia amechukua uamuzi huo ili kuhakikisha kwamba fedha zilizopangwa kutumika kuadhimisha miaka 61 ya uhuru, zinaleta tija kwa jamii.

Amesema tayari fedha hizo zimeshapelekwa katika Wizara ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI, kwa ajili ya utekelezaji.

“Hivyo sherehe za mwaka huu hakutakuwa na gwaride wala shughuli nyingine za kitaifa ambazo zitafanyika kwenye uwanja au mahala pamoja,” amesema Simbachawene.

Ametaja shule za wanafunzi wenye mahitaji maalum zitakazonufaika kuwa ni, Buhangija iliyoko Shinyanga, Goweko (Tabora), Darajani (Singida), Mtanga (Lindi), Songambele (Manyara), Msanzi (Rukwa), Idofi (Njombe) na Longido (Arusha).

Aidha, Simbachawene amesema sherehe za maadhimisho hayo yenye kauli mbiu ya “miaka 61 ya uhuru, amani na umoja ni nguzo ya maendeleo yetu”, yatafanyika kupitia makongamano mbalimbali yatakayofanyika katika mikoa na wilaya za Tanzania Bara.

“Makongamano yatatumika kujadili, kutafakari na kukumbuka tulipotoka, tulipo na tunapoelekea kuhusu maendeleo endelevu ambayo nchi yetu imeyapitia na kuyafikia. Kufanya shughuli za kijamii ikiwemo kufanya usafi maeneo ya kijamii, hospitali, nyumba za wazee na makundi maalum,” amesema Simbachawene.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!