Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari Dk. Salim afikisha miaka 80, marais Samin Ramaphosa wamtakia kheri
Habari

Dk. Salim afikisha miaka 80, marais Samin Ramaphosa wamtakia kheri

Spread the love

 

MWANADIPLOMASIA mashuhuri nchini Tanzania, Dk. Salim Ahmed Salim leo Jumapili, tarehe 23 Januari 2022, ametimiza miaka 80 tangu alipozaliwa. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Dk. Salima aliyewahi kuwa waziri mkuu wa Tanzania na Katibu Mkkuu wa Umoja wa Nchi Huru Afrika (OAU) ambayo sasa ni Umoja wa Afrika (AU) alizaliwa tarehe 23 Januari 1942, visiwani Zanzibar.

Viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya Tanzania, wamemtakia kheri mwanadiplomasia huyo ambaye kwa sasa anakabiliwa na tatizo la kiafya.

Katika ukurasa wake wa Twitter, Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameweka picha ya Dk. Salima na kuandika, “Kheri ya siku ya kuzaliwa kwa Mheshimiwa Dkt. Salim Ahmed Salim, mtumishi mahiri wa umma wa Watanzania, Afrika na Dunia kwa zaidi ya miongo minne.”

“Katika siku hii adhimu ya kumbukumbu ya miaka 80 ya kuzaliwa kwako, tunakushukuru kwa utumishi uliotukuka kwa nchi yetu.

Naye Cyril Ramaphosa, Rais wa Afrika Kusini amempongeza na kumtakia kheri Dk. Salim akimwelezea kama mmoja wa kiongozi mashuhuri wa kuleta umoja barani Afrika, “na rafiki wa kweli kwa wananchi wa Afrika Kusini.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!