DAKTARI Faustine Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni anayemaliza muda wake amesema, bado ana mikakati ya kuendelea kutatua changamoto ndani ya jimbo hilo. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).
Dk. Ndugulile amesema hayo leo Jumatatu tarehe 20 Julai 2020 katika mkutano mkuu wa jimbo la Kigamboni wenye lengo la kupiga kura za maoni kumpata mgombea ubunge.
Katika kitabu cha wagombea, Dk. Ndugulile anayetetea nafasi hiyo ni mgombea namba 58 kati ya 78 wanaowania kupeperusha bendera ya CCM katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020.
Soma zaidi:
Akijinadi mbeye ya wajumbe wa mkutano huo unaofanyikia ukumbi wa Chuo cha Mwalimu Nyerere, Kuvukoni amesema, “mlinipa imani ya kuwa mbunge na nikawapa utumishi na sasa nawahakikishia tena mnipe imani ili niwape tena utumishi. Msiache mbachao kwa msala upitao,” amesema.
Ameeleza mbele ya wajumbe hao kuwa katika kipindi cha uongozi wake, amefanikiwa kujenga mfumo nzuri wa afya pamona na elimu katika jimbo na kuwa katika matokeo ya shule ya msingi ya mwaka huu Kigamboni imeshika nafafi ya 10 kitaifa.
“Nakiri kwamba, pamoja na yote yaliyofanyika bado kuna changamoto mbalimbali na bado nina mikakati ya kuzitatua,” amesema.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari zaidi
isayaemanuel22@gmail.com