Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Maisha Afya Dk. Ndugulile atembelea MOI, akagua chumba cha tiba mtandao
Afya

Dk. Ndugulile atembelea MOI, akagua chumba cha tiba mtandao

Dk. Faustine Ndungulile, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (katikati) akikagua wodi ya kutibu kwa mtandao
Spread the love

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulile ametembelea Taasisi ya Tiba ya mifupa, upasuaji wa ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu (MOI) kukagua maendeleo ya chumba maalum cha Tiba mtandao ambacho kinatarajia kukamilika na kufanya kazi kuanzia mwezi Juni mwaka huu. Anaripoti Hamisi Mguta … (endelea).

Awali akiwa kwenye taasisi hiyo ya MOI, Dk. Ndugulile aliweza kupokea maendeleo ya ukamilishwaji wa chumba hicho cha tiba mtandao ambapo pia aliwataka kuhakikisha wanasimamia vizuri uendeshaji wake kwani utasaidia Taifa kutoa huduma za kibingwa sehemu kubwa zaidi hapa nchini zikiwemo hospitali za rufaa za mikoa na nyingine 

Aidha, Dk. Ndugulile amewataka kukamilisha hatua zote za chumba hicho na kitakapokamilika uzinduzi ufanyike kama inavyotarajiwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Dk. Respicious Boniface amesema kuwa, chumba hicho kinategemea kukamilika na kuanza kufanya kazi mwezi Juni mwaka huu na kitakapokamilika kitasaidia matibabu kwa kwa njia ya mtandao nchi nzima.

“Chumba cha Tiba mtandao hapa MOI kitakapokamilika hospitali zote kubwa za rufaa za mikoa na zingine za Rufaa, zitatuma picha hapa na watalaam wa MOI wanatoa majibu na kurudisha tiba kule na kutoa ushauri wa jinsi wa kutoa matibabu kwa wagonjwa wakiwa hukohuko,” alieleza Dk. Boniface.

Chumba hicho cha tiba mtandao kinatarajiwa kuwepo kwenye jengo jipya la MOI ambapo tayari timu ya watalaam wanaendelea na taratibu za kukamilisha uendeshaji wake.

MOI ni miongoni mwa Taasisi za tiba zenye kutoa huduma za kibingwa huku ikiwa na Madaktari wabobezi kwenye tiba ya mifupa, upasuaji wa ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi GGML wajitokeza kuchunguzwa saratani

Spread the loveWAFANYAKAZI wa Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) leo...

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML yatoa msaada wa vifaa tiba kuboresha afya Geita

Spread the loveKATIKA jitihada za kuendelea kuboresha sekta ya afya mkoani Geita,...

Afya

Hospitali Kanda Mtwara yaokoa mamilioni, yajipanga kuhudumia nchi jirani

Spread the love  MAMILIONI ya fedha yaliyopaswa kutumika katika kusafirisha wagonjwa kutoka...

AfyaHabari Mchanganyiko

Magonjwa yasiyoambukiza tishio, vyombo vya habari vyatakiwa kuelimisha umma

Spread the loveVYOMBO vya habari vimetakiwa kuongeza jitihada katika elimu ya kujikinga...

error: Content is protected !!