Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Ndugulile aendelea ‘kulilia’ vivuko Kigamboni
Habari za Siasa

Dk. Ndugulile aendelea ‘kulilia’ vivuko Kigamboni

Kivuko cha MV Magogoni
Spread the love

 

MBUNGE wa Kigamboni jijini Dar es Salaam kupitia chama tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Faustine Ndugulile amesema, kilio cha ubovu wa vivuko kwa wananchi wa Kigamboni ni cha muda mrefu na jitihada za haraka zinahitajika kufanyika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Dk. Ndugulile kwa kipindi kirefu amekuwa akizungumzia kero hiyo ambayo inasababishwa na vivuko hivyo kutoa huduma kwa kusuasua kwa baadhi kuharibika hivyo kusababusha adha kwa wananchi.

Hivi karibuni, akiwa bungeni jijini Dodoma alishauri kama Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) imeshindwa kuvisimamia ivibinafsishwe.

Dk. Faustin Ndungulile, Mbunge wa Kigamboni

Leo Alhamisi tarehe 2 Juni 2022, ametumia ukurasa wa kijamii wa Twitter kuweka picha ya kivuko na umati wa wananchi huku akiandika, “hatua za haraka zinahitajika kunusuru hali hii.”

“Tusisubiri maafa halafu tuunde Tume. Kama TEMESA imeshindwa, huduma hii ibinafsishwe. Wana Kigamboni wanastahili huduma bora, salama na ya uhakika ya vivuko. Ni haki na sio hisani.”

1 Comment

  • Asante.ndugulile lakini uwelewe mamlaka husika maelezo yako hawana shughuri nayo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!