Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Mwinyi: Tanzania inatambua umuhimu wa vyombo vya habari
Habari Mchanganyiko

Dk. Mwinyi: Tanzania inatambua umuhimu wa vyombo vya habari

Spread the love

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua umuhimu Vyombo wa Habari, kwani kupitia vyombo hivyo wananchi wanapata taarifa mbalimbali za shughuli za Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar …(endelea).

Dk. Mwinyi amesema hayo jana tarehe 3 Mei 2023 Visiwani Zanzibar wakati wa kilele Miaka 30  ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, ambayo kwa mara ya kwanza yamefanyika visiwani humo.

“Tanzania inatambua umuhimu wa vyombo vya habari, kupitia vyombo vya habari wananchi wamejua shughuli zinazofanywa na Serikali, vilevile kutoa elimu kwa wananchi juu ya masuala mbalimbali ya maendeleo, kama vile masuala ya kilimo na shughuli nyingine za kujikwamua kiuchumi,” amesema Dk. Mwinyi.

Ameendelea kusema kuwa, vyombo habari vimewasaidia wanasiasa, kutangaza sera za vyama vyao kwa wananchi, hivyo kufahamu mipango mbalimbali ya vyama vya siasa pamoja.

Aidha, Dk. Mwinyi ametoa wito kwa waandishi wa habari kuwa wazalendo na nchi yao kwani hakuna Uhuru usio na mipaka, wala  uhuru usio na wajibu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!