Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwinyi kuapishwa J’3 ijayo, Dk. Magufuli Novemba 5
Habari za Siasa

Dk. Mwinyi kuapishwa J’3 ijayo, Dk. Magufuli Novemba 5

Dk. Hussein Mwinyi, mshindi wa Urais Zanzibar akionesha hati ya ushindi
Spread the love

RAIS Mteule wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi anatarajiwa kuapishwa Jumatatu ijayo ya tarehe 2 Novemba 2020, katika Viwanja vya Amani visiwani humo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 31 Oktoba 2020 na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole wakati anazungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

“Ningependa kusisitiza siku ya Jumatatu kule Zanzibar Wazanzibar wote na Watanzania wote wenye mapenzi mema na demokrasia wajitokeze kwa wingi Viwanja vya Amani ambapo ndugu yetu ataaapishwa kuwa rais wa Serikali ya Mapinduzi  ya Zanzibar awamu ya nane. Hivyo shime Watanzania wote mjitokeze kwenda kushuhudia tukio hilo,” amesema Polepole.

Dk. Mwinyi aliyekuwa Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020, alishinda kiti hicho kwa kupata asilimia 76.27 ya kura huku aliyekuwa mpinzani wake karibu kupitia ACT-Wazalendo,  Maalim Seif sharif Hamad  akipata asilimia 19.87.

Rais John Magufuli

Polepole amesema sherehe hiyo ya uapisho itaongozwa na Rais Mteule, Dk. John Magufuli na Rais wa Zanzibar anayemaliza muda wake, Dk. Ali Shein.

Wakati Dk. Mwinyi akitarajia kuapishwa siku ya Jumatatu ijayo, Dk. Magufuli anatarajia kuapishwa tarehe 5 Novemba 2020 katika Viwanja vya Jamhuri jijini  Dodoma.

“Tarehe 5 Novemba 2020 katika viwanja vya Jamhuri Dodoma taarifa inatolewa kwa Watanzania wote kutafanyika tukio lingine kubwa la kihistoria ambapo ndugu yetu John Magufuli ataapishwa kule Dodoma.  Shime  karibuni sana viwanja vya Jamhuri tukashuhudie uongozi wa kidemokrasia Tanzania,” amesema Polepole.

Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM

Jana tarehe 30 Oktoba 2020 Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilimtangaza Dk. Magufuli aliyekuwa mgombea urais wa Tanzania wa CCM kushinda uchaguzi huo baada ya kupata kura milioni 12.5 kati ya milioni 15.9 zilizopigwa, wakati aliyekuwa mpinzani wake kupitia chama cha Chadema, Tundu Lissu akipata kura milioni 1.9.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!