RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.Hussein Ali Mwinyi leo Jumatano tarehe 4, Januari, 2023, ameshuhudia utiaji saini wa makubaliano ya ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Pemba.
Makubaliano hayo yamesainiwa kati ya Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi na Uongozi wa Kampuni ya Propav kutoka Brazil, pamoja na Mecco ya Tanzania, pia Ujenzi wa barabara za Chake-Mkoani Pemba, Unguja- Tunguu-Makunduchi na Fumba-Kisauni. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Halfa hiyo imefanyika Ikulu na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Kitaifa wa Serikali,Chama ,wa dini na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama.
Leave a comment