Friday , 9 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwigulu: Viwanda vipya 8,477 vimejengwa
Habari za Siasa

Dk. Mwigulu: Viwanda vipya 8,477 vimejengwa

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imeeleza, katika kipindi cha miaka mitano (2019-2020), jumla ya viwanda vipya 8,477 vimejengwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kati ya hivyo, vikubwa ni 201, vya kati 460, vidogo 3,406 na vidogo zaidi 4,410, na kwamba ujenzi wa viwanda hivyo umeongeza idadi ya viwanda nchini kutoka 52,633 mwaka 2015 hadi viwanda 61,110.

Ni kauli ya Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango aliyoitoa leo Alhamisi tarehe 7 Aprili 2021, bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/22 – 2025/26).

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango

“Viwanda hivyo vimechangia ongezeko la uzalishaji wa bidhaa mbalimbali katika soko la ndani na la nje ikijumuisha bidhaa za ngozi, nguo, ujenzi (nondo, mabati, saruji, misumari, marumaru na rangi), plastiki, zana za kilimo na vinywaji.”

“Uwekezaji huo umeleta mafanikio yafuatayo: Kuongezeka kwa mchango wa Sekta ya Viwanda katika Pato la Taifa kutoka asilimia 7.9 mwaka 2015 hadi asilimia 8.5 mwaka 2019; kukua kwa sekta ya uzalishaji viwandani kwa wastani wa asilimia 8.3.

Akitaja mafanikio mengine amesema, viwanda hivyo vimesaidia kuzalishwa fursa za ajira kutoka ajira 254,786 mwaka 2015 hadi ajira 482,601 mwaka 2019 na kuchangia katika mapato yatokanayo na mauzo ya bidhaa nje ya nchi kutoka asilimia 13.8 mwaka 2016/17 hadi asilimia 14.2 mwaka 2019/20.

Amesema, katika kipindi cha utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo, Sh. 45.3 bilioni kimetumika kuchochea miradi ya uzalishaji viwandani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!