Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwigulu: Viwanda vipya 8,477 vimejengwa
Habari za Siasa

Dk. Mwigulu: Viwanda vipya 8,477 vimejengwa

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imeeleza, katika kipindi cha miaka mitano (2019-2020), jumla ya viwanda vipya 8,477 vimejengwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kati ya hivyo, vikubwa ni 201, vya kati 460, vidogo 3,406 na vidogo zaidi 4,410, na kwamba ujenzi wa viwanda hivyo umeongeza idadi ya viwanda nchini kutoka 52,633 mwaka 2015 hadi viwanda 61,110.

Ni kauli ya Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango aliyoitoa leo Alhamisi tarehe 7 Aprili 2021, bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/22 – 2025/26).

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango

“Viwanda hivyo vimechangia ongezeko la uzalishaji wa bidhaa mbalimbali katika soko la ndani na la nje ikijumuisha bidhaa za ngozi, nguo, ujenzi (nondo, mabati, saruji, misumari, marumaru na rangi), plastiki, zana za kilimo na vinywaji.”

“Uwekezaji huo umeleta mafanikio yafuatayo: Kuongezeka kwa mchango wa Sekta ya Viwanda katika Pato la Taifa kutoka asilimia 7.9 mwaka 2015 hadi asilimia 8.5 mwaka 2019; kukua kwa sekta ya uzalishaji viwandani kwa wastani wa asilimia 8.3.

Akitaja mafanikio mengine amesema, viwanda hivyo vimesaidia kuzalishwa fursa za ajira kutoka ajira 254,786 mwaka 2015 hadi ajira 482,601 mwaka 2019 na kuchangia katika mapato yatokanayo na mauzo ya bidhaa nje ya nchi kutoka asilimia 13.8 mwaka 2016/17 hadi asilimia 14.2 mwaka 2019/20.

Amesema, katika kipindi cha utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo, Sh. 45.3 bilioni kimetumika kuchochea miradi ya uzalishaji viwandani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!