Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Mpango atoa maelekezo saba matumizi ya Kiswahili
Habari Mchanganyiko

Dk. Mpango atoa maelekezo saba matumizi ya Kiswahili

Makamu wa Rais, Dk. Philip Mpango
Spread the love

 

MAKAMU wa Rais Dk. Philip Mpango ametoa maelekezo saba kwa Wizara na taasisi mablimbali nchini katika kuhakikisha Kiswahili kinatumika ipasavyo katika shughuli mbalimbali za serikali. Anaripoti Jonas Mushi, Dar es Salaam … (endelea).

Ametoa maagizo hayo leo Alhamisi tarehe 7 Julai, 2022, katika sherehe za maadhimisho ya siku ya Kiswahili duniani zilizofanyika kitaifa jijini Dar es Salaam.

Dk. Mpango ameziagiza Wizara na taasisi za serikali kuendelea kutekeleza maagizo ya serikali yaliyokwisha kutolewa kwamba nyaraka za mawasiliano za wizara na idara zake ziwe kwa lugha ya Kiswahili. Pia mikutano, warsa, semina mijadala ya umma na dhifa ziendeshwe kwa Kiswahili.

Makamu huyo wa Rais pia ameagiza majina ya barabara mitaa, mabango fomu za usahili na maelekezo ya dawa zote na bidhaa na huduma ziandikwe kwa Kiswahili.

Mbali na hayo ameelekeza taarifa za miradi na mikataba inayohusu wananchi “lazima” iwe kwa Kiswahili “isiwe kwa lugha za kigeni pekee,” na kusema lengo ni kuhakikisha kila mwananchi anaelewa jambo linalohusu ustawi wa maisha yake.

Vilevile ameelekeza Sheria na kanuni ambazo bado hazijatafsiriwa zitafsiriwe na Wizara na Taasisi zinazosimamia sheria na kanuni hizo, kwa kushirikiana na mabaraza ya Kiswahili, wataalamu wengine wa Kiswahili na Ofisi ya Mwanasehria mkuu wa Serikali.

Pia ameagiza vyombo vya habari vinavyotumia Kiswahili “vihakikishe” vinatumia Kiswahili fasaha na sanifu, huku “vikizingatia kwa dhati” sarufi ya Kiswahili.

Aidha, pale anaposhirikishwa mtu anayeongea lugha isiyokuwa Kiswahili, ameelekeza chombo cha habari husika “kitoe tafsiri ya maneno yasiyo ya Kiswahili ili wananchi waelewe kinachozungumzwa.”

Dk. Mpango amesisitiza agizo lililotolewa na Rais Samia kwa balozi zote za Tanzania kuanzisha vituo vya kufunzia lugha ya Kiswahili.

“Na hapa napenda niagize balozi zote ziwatumie wataalamu wa Kiswahili walio sajiliwa kwenye kanzi data ya BAKITA na BAKIZA-Dk,” amesema Dk. Mpango.

Maelekezo mengine ni BAKITA na BAKIZA kuwa wabunifu katika kuzalisha misamiati ya Kiswahili ili kuendana na kasi ya maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia na Wizara na taasisi husika kuhakikisha mfumo wa kufundisha Kiswahili kwa wageni kwa njia ya mtandao Swahili Prime unatumika kikamilifu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!