Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Mpango aitaka TFS idhibiti vibali vya ukataji misitu
Habari Mchanganyiko

Dk. Mpango aitaka TFS idhibiti vibali vya ukataji misitu

Misitu ya Sao Hill, iliyoko Mufindi mkoani Iringa
Spread the love

 

MAKAMU wa Rais, Dk. Phillip Mpango, ameutaka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), kupitia upya sheria za utoaji vibali vya kuvuna mazao ya misitu, ili kudhibiti ukataji holela wa miti kwa ajili ya shughuli za kibinadamu hususan mkaa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Dk. Mpango alitoa agizo hilo tarehe 12 Januari 2023, katika kilele cha upandaji miti kilichoendana na kumbukumbu ya miaka 59 ya mapinduzi ya Zanzibar, jijini Dodoma.

“Ikibidi mpitie upya sheria za utoaji wa vibali vya kuvuna mazao ya misitu ambavyo vitawezesha utunzaji wa mazingira kwa lengo la kuboresha mazingira kwa kuongeza wingi wa kupanda miti,” alisema Dk.Mpango.

Katika hatua nyingine, Dk. Mpango aliagiza Halmashauri ya Jiji la Dodoma, kuwapa adhabu kali ikiwemo faini, watu watakaokutwa na makosa ya kufanya uharibifu wa mazingira.

Wakati huo huo, Dk. Mpango aliziagiza halmashauri zote nchini kupanda miti isiyopungua milioni 1.5, kwa ajili ya kuhamasisha utunzaji wa mazingira kwa wananchi.

3 Comments

  • Wangeweka utaratibu ambao hauumizi mwanaichi na siyo sheria ipitiwa upya na uamuzi hapo hapo bira kuwasikiriza wanachi mimi ni najishugurisha na kusafirisha mkaa reseni ya kusafirishia ninayo na kibari nakatia ira tumesimamishwa gafura na tunamikopo na mikataba ya pikipiki tunavunia kibaha na kureta dar wengeweka utaratibu na siyo gafra ivo

  • Naombeni vyombo vya habari wariingirie kati sheria ipitiwe na kazi ienderee uamuzi ukipatikana taratibu zitafatwa na kazi ziendere tupewe muda nipo bunju

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!