Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Magufuli: Sikustahili urais
Habari za Siasa

Dk. Magufuli: Sikustahili urais

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amesema kuwa, hakustahili kuwa Rais wa Tanzania bali Watanzania wenyewe ndio waliomchagua. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Amesema, wananchi wa Mbarali mkoani Mbeya na maeneo mengine ya nchi, ndio walimuona anafaa kushika wadhida huo kati ya wale waliokuwa wanagombea.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo tarehe 2 Aprili 2019, wakati akituhutubia mkutano wa hadhara mjini Mabarali akiwa kwenye mwendelezo wake wa ziara ya siku nane.

Akihutubia kwenye mkutano huo, Rais Magufuli amesema hakustahili kuwa rais, bali wananchi wa Tanzania walikuwa na sababu za msingi za kumchagua.

Na kwamba, Watanzania waliamua kumchagua kwa kuwa, waliamini anaweza kutatua matatizo yao hasa ya wanyonge.

“Mlinichagua kuwa kiongozi wenu, sikustahili kuwa Rais, mliamua kuwa Magufuli tunampa urais. Sasa tuna miaka mitatu kwenye uongozi na tuliahidi kutekeleza Ilani ya CCM, mawaziri wameeleza tuliyofanya na ambayo bado hayajafanyika wameeleza changamoto zake,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!