Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Kigwangalla, Makonda wavaana, kisa picha ya JPM
Habari za Siasa

Dk. Kigwangalla, Makonda wavaana, kisa picha ya JPM

Spread the love

MUDA mfupi baada ya Paul Makonda, kuandika kwenye ukurasa wake wa Instagram, akimtaka mchekeshaji Idrisa Sultan ‘kujisalimisha’ katika kituo chochote cha polisi kwa madai ya kuvuka mipaka, Dk. Hamisi Kigwangalla ameibuka na kuahidi kumtetea. Anaripoti Martin Kamote … (endelea).

Makonda ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, anamtuhumu Idriss kuvuka mipaka yake ya kazi, kwa kuchapisha picha ya Rais John Magufuli iliyohaririwa kisha na kuambatanisha ujumbe unaosomeka “kwa siku moja tukabadilishana kazi ili a-enjoy birthday yake kwa amani.”

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Dk. Kigwangalla amesema, iwapo Idriss atakamatwa na polisi kuhusiana na tuhuma hizo, atampatia mwanasheria wa kumtetea pamoja na kumuwekea dhamana.

“Nimeambiwa kuna msanii wa vichekesho anatafutwa na polisi, akikamatwa mniambie, nitajitolea mwanasheria wa kwenda kumuwekea dhamana na kumtetea. Rais wetu ni mtu wa watu na imejidhihirisha kwa jinsi wananchi walivyojitolea kumuombea dua siku ya kuzaliwa kwake! Wameonesha upendo,” ameandika Dk. Kigwangalla.

Andiko la Dk. Kigwangala, Waziri wa Maliasili na Utalii linapuuza kile alichoandika Makonda “naona mipaka ya kazi yako huijui. Nenda sasa hivi kituo chochote cha polisi uwambie Makonda kaniambia nije, utakuta ujumbe wako.”

Idrisa ameandika ujumbe huo siku moja baada ya Rais Magufuli kusheherekea kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa tarehe 29 Oktoba 1959.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!