Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari Dk. Kalemani aipa maagizo TANESCO
Habari

Dk. Kalemani aipa maagizo TANESCO

Dk. Medard Kalemani
Spread the love

WAZIRI wa Nishati, Dk. Medard Kalemani ameliagiza Shirika la Umeme wa Ugavi nchini (TANESCO), kuhakikisha umeme haukatiki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Pia amelitaka shirika hilo kutoa taarifa pale linapolazimika kukata umeme kwa sababu za msingi na kuurejeshwa kwa haraka.

“Pale mnapolazimika kukata umeme kwa sababu za msingi, itolewe taarifa,” amesema Dk. Kalemani na kuongeza “..na umeme urejeshwe muda ulioandikwa kwenye taarifa hiyo.”

Dk. Kalemani ametoa maagizo hayo wakati alipokutana na wakuu wa Taasisi na Menejimenti za Wizara ya Nishati, jijini Dodoma.

Waziri huyo amezitaka taasisi hizo kuhakikisha miradi inayosimamiwa na wizara hiyo inakamilika kwa wakati.

Pia amesema, licha ya kukamilika kwa wakati anataka kuona miradi hiyo inakamilika kwa ubora ulinaokubalika na si vinginevyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!