Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Hussein: Kupata ushindi Z’bar ni ngumu
Habari za Siasa

Dk. Hussein: Kupata ushindi Z’bar ni ngumu

Maalim Seif Sharrif Hamad, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
Spread the love

KAZI ya kuutafuta ushindi kwenye uchaguzi mkuu visiwani Zanzibar ni ngumu. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Hiyo ni kauli ya Dk. Hussein Mwinyi, mgombea urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), aliyoitoa baada ya kuchaguliwa na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho leo tarehe 10 Julai 2020.

Kwenye uchaguzi huo, Dk. Mwinyi amechaguliwa kwa kura 129 (asilimia 78.65), Shamsi Vuai Nahodha akipata kura 16 (asilimia 9.76) na Dk. Khalid Salum Muhamed akipata kura 19 (asilimia 11.58).

          Soma zaidi:-

Dk. Mwinyi amewaeleza wajumbe wa NEC, kwamba kazi iliyoko mbele ni kubwa, lakini anaamini atafanikiwa kwa kuwa haitakuwa kazi ya peke yake, bali ya WanaCCM wote.

Dk. Hussein Mwinyi

“Lakini leo tumemaliza namshukuru Mungu huku nikijua kwamba kazi iliyokuwa mbele ni kubwa zaidi, lakini nafarijika kwamba haitakuwa yangu peke yangu ni yetu sote,” amesema Dk. Mwinyi.

Amesema, kinyang’anyiro cha uteuzi wa mgombea Urais wa Zanzibar, kilikuwa sawa na mtihani mkubwa kwake, lakini anamshukuru Mungu kwamba amefaulu.

“Zoezi hili halikuwa rahisi, mimi katika maisha yangu nimefanya mitihani mingi lakini mkubwa ulikuwa huu.  Mkiniona napungua ni kwa sababu hii,” amesema Dk. Mwinyi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!