Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Hoseah, wenzake waapishwa TLS
Habari MchanganyikoTangulizi

Dk. Hoseah, wenzake waapishwa TLS

Dk. Edward Hoseah, Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika akiapa kushika nafasi hiyo
Spread the love

 

DAKTARI Edward Hoseah, ameapishwa kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), akimrithi Dk. Rugemeleza Nshala, aliyemaliza muda wake. Anaripoti Regina Mkonde, Arusha … (endelea).

Dk. Hoseah ameapishwa leo Jumamosi tarehe 17 Aprili 2021, na Corman Ngaro, Wakili Mwandamizi TLS, katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), jijini Arusha.

Rais huyo mpya wa TLS, ameapishwa baada ya kushinda kiti cha Urais katika Uchaguzi Mkuu wa chama hicho, uliofanyika jana Ijumaa tarehe 16 Aprili 2021 katika Viwanja vya AICC.

Dk. Hoseah alishinda kwa kura 293 kati ya kura 802 zilizopigwa na mawakili walioshiriki uchaguzi huo.

Dk. Hoseah aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), aliwashinda wagombea wenzake wanne, Flaviana Charles (223), Francis Stolla (17), Shehzada Walli (192) na Albert Msando (69).

Viongozi mbalimbali wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) wakiapa

Mbali na uapisho wa Dk. Hoseah, Pia, Gloria Kabalamu, naye ameapishwa kuwa Makamu wa Rais wa TLS.

Wengine walioapishwa ni, Dk. Fauz Twaib na Rwekama Rweikiza, ambao wameapishwa kuwa viongozi wa Bodi ya Mali za TLS.

Naye Capt. Ibrahim Bendera, ameapishwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Mawakili wa TLS.

Hali kadhalika, wajumbe wa Baraza la Uongozi la TLS nao pia waliapishwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!