Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Dk. Hoseah atakiwa kulinda heshima TLS
Habari Mchanganyiko

Dk. Hoseah atakiwa kulinda heshima TLS

Dk. Rugemeleza Nshala, Rais wa TLS anayemaliza muda wake, akimkabidhi ofisi, Rais mpya, Dk. Edward Hoseah
Spread the love

 

DAKTARI Rugemeleza Nshala, Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika aliyemaliza muda wake, amemtaka mrithi wake, Dk. Edward Hoseah, ailinde heshima ya chama hicho, aliyoiacha. Anaripoti Regina Mkonde, Arusha … (endelea).

Dk. Nshala ametoa wito huo leo Jumamosi tarehe 17 Aprili 2021, wakati akiaga katika mkutano mkuu wa chama hicho, uliofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), jijini Arusha.

Rais huyo mstaafu wa TLS, amewaaga mawakili wa chama hicho, baada ya muda wake wa uongozi wa miaka mwili (Aprili 2019-Aprili 2021), kumalizika kufuatia uchaguzi mkuu uliofanyika Ijumaa tarehe 17 Aprili 2021 na kumuingiza madarakani Dk. Hoseah.

Akiaga katika mkutano huo, Dk. Nshala amesema, yeye na uongozi uliomaliza muda wake, wanaiacha TLS ikiwa imara, hali iliyothibitishwa na muitikio mkubwa ndani na nje ya nchi, kuufuatilia uchaguzi huo.

“Tumejitahidi kusukuma gurudumu hili tulipoweza, tumelinda heshima ya chama chetu kama mlivyoona jana, uchaguzi wetu umefuatiliwa na watu dunia nzima, hii inaonesha hiki si chama cha hovyo hovyo. Ni chama chenye heshima kubwa sana wanaokuja waendelee kuilinda,” amesema Dk Nshala, Rais TLS.

Dk. Nshala amewaahukuru wanachama wa TLS kwa kumchagua kuwa rais wao.

“Nashukuru tumeweza kufika mwisho wa uongozi wetu, mwisho wa siku tumefanya uchaguzi na kuimarisha demokrasia katika chama chetu.”

“Asanteni kwa heshima mliyotupa kuwaongoza, tuzidi kushikamana na kuwatakia kila la kheri, wanaokuja waweze kuliendeleza hili gurudumu mbele,” amesema Dk. Nshala.

Dk. Hoseah ataiongoza TLS kwa muda wa mwaka mmoja kuanzia Aprili 2021 hadi Aprili 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!