Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Hoseah atakiwa kulinda heshima TLS
Habari Mchanganyiko

Dk. Hoseah atakiwa kulinda heshima TLS

Dk. Rugemeleza Nshala, Rais wa TLS anayemaliza muda wake, akimkabidhi ofisi, Rais mpya, Dk. Edward Hoseah
Spread the love

 

DAKTARI Rugemeleza Nshala, Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika aliyemaliza muda wake, amemtaka mrithi wake, Dk. Edward Hoseah, ailinde heshima ya chama hicho, aliyoiacha. Anaripoti Regina Mkonde, Arusha … (endelea).

Dk. Nshala ametoa wito huo leo Jumamosi tarehe 17 Aprili 2021, wakati akiaga katika mkutano mkuu wa chama hicho, uliofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), jijini Arusha.

Rais huyo mstaafu wa TLS, amewaaga mawakili wa chama hicho, baada ya muda wake wa uongozi wa miaka mwili (Aprili 2019-Aprili 2021), kumalizika kufuatia uchaguzi mkuu uliofanyika Ijumaa tarehe 17 Aprili 2021 na kumuingiza madarakani Dk. Hoseah.

Akiaga katika mkutano huo, Dk. Nshala amesema, yeye na uongozi uliomaliza muda wake, wanaiacha TLS ikiwa imara, hali iliyothibitishwa na muitikio mkubwa ndani na nje ya nchi, kuufuatilia uchaguzi huo.

“Tumejitahidi kusukuma gurudumu hili tulipoweza, tumelinda heshima ya chama chetu kama mlivyoona jana, uchaguzi wetu umefuatiliwa na watu dunia nzima, hii inaonesha hiki si chama cha hovyo hovyo. Ni chama chenye heshima kubwa sana wanaokuja waendelee kuilinda,” amesema Dk Nshala, Rais TLS.

Dk. Nshala amewaahukuru wanachama wa TLS kwa kumchagua kuwa rais wao.

“Nashukuru tumeweza kufika mwisho wa uongozi wetu, mwisho wa siku tumefanya uchaguzi na kuimarisha demokrasia katika chama chetu.”

“Asanteni kwa heshima mliyotupa kuwaongoza, tuzidi kushikamana na kuwatakia kila la kheri, wanaokuja waweze kuliendeleza hili gurudumu mbele,” amesema Dk. Nshala.

Dk. Hoseah ataiongoza TLS kwa muda wa mwaka mmoja kuanzia Aprili 2021 hadi Aprili 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!