Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Hoseah anavyojipanga kuongoza TLS, atoa ushauri Takukuru, DPP
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Hoseah anavyojipanga kuongoza TLS, atoa ushauri Takukuru, DPP

Dk. Edward Hoseah, mgombea Urais TLS
Spread the love

 

TAREHE 15 Aprili 2021, Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kitafanya uchaguzi mkuu wa viongozi mbalimbali ikiwemo urais, watakaoongoza chama hicho kwa mwaka mmoja. Anaripoti Matrida Peter…(endelea).

Wanachama watano wamejitosa kuwania nafasi hiyo ya urais ambao ni; Albert Msando, Francis Stolla, Flaviana Charles, Shehzada Walli na Dk. Edward Hoseah.

MwanaHALISI TV limefanya mahojiano maalum na Dk. Hoseah, aliyewahi kuhudumu nafasi mbalimbali ndani ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kuanzia mwaka 1995 hadi 2015, ikiwemo ya mkurugenzi mkuu.

Katika mahojiano hayo, Dk. Hoseah amezungumzia masuala mbalimbali, kama vile kilichomsukuma kuwania nafasi hiyo, anachotaka kukifanya TLS, anavyojitofautisha na wagombea wenzake.

Dk. Hoseah, anavyotizama suala la haki, uadilifu na utu, nini Takukuru wanapaswa kukifanya ili kuwa na kesi zenye mashiko na ushahidi wenye tija bila kuwaweka watuhumiwa mahabusu kwa muda mrefu, ushauri wake kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Anazungumzia jinsi misimamo yake hususan kusimamia kanuni, unavyowashinda baadgi ya watu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!