Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Dk. Gwajima aipa siku 10 MOI
Afya

Dk. Gwajima aipa siku 10 MOI

Spread the love

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Dorothy Gwajima, ametoa siku 10 kwa Taasisi ya Tiba na Mifupa Muhimbili (MOI), iwasilishe changamoto zake, kwa ajili ya kutafutiwa ufumbuzi. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaa…(endelea).

Dk. Gwajima alitoa maelekezo hayo jana tarehe 17 Julai 2021, alipozungumza na uongozi wa MOI, jijini Dar es Salaam.

Waziri huyo wa afya alitoa maelekezo hayo, baada kubaini taasisi hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali, zinazoikwamisha kutoa huduma kwa wananchi.

Aidha, Dk. Gwajima ameipongeza MOI kwa kendelea kutoa huduma bora kwa Watanzania, kwa zaidi ya miaka 25 tangu ilipoanzishwa.

“ Hongereni mnafanya kazi nzuri, nimekuja hapa tujadiliane ili tuone ni namna gani MOI itafikisha miaka 30 ikiwa bora Zaidi, kueni huru kuchangia mada ili tusonge mbele Zaidi.” Alisema Dk. Gwajima

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini MOI, Prof. Charles Mkonyi, alisema hiyo ina mpango wa kuanzisha kliniki katika wilaya za Mkoa wa Dar es Salaam, ili wananchi wapate huduma.

“Pamoja na kuanzisha hizi kliniki, pia tunalenga kujenga hospitali ya kisasa ya utengamano, katika kiwanja cha MOI kilichopo Mbweni Mpiji jiji Dar es. Salaam, Alisema Prof. Mkonyi.

Naye Mkurugenzi mtendaji wa MOI, Dk. Respicious Boniface alisema taasisi hiyo imeendelea kusogeza huduma kwa wananchi wa mikoani, ili kuwapunguzia adha ya kusafiri kufuata huduma Dar es Salaam.

“Tumesogeza huduma za kibingwa za ubongo KCMC pamoja na Bugando tumesogeza huduma za Mifupa, Hospiali ya kanda Mbeya na Nyangao Lindi Alisema Dk. Boniface.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!