Friday , 9 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Bashiru: Nape, Bashe ni watu muhimu CCM
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Bashiru: Nape, Bashe ni watu muhimu CCM

Spread the love

NAPE Nnauye, Mbunge wa Mtama na Hussein Bashe, Mbunge wa Nzega Mjini ni miongoni mwa wanasiasa vijana wanaomvutia Dk. Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akimzungumzia Nape katika mahojiano maalum na Kituo cha Televisheni cha ZBC2 leo tarehe 26 Aprili 2019, Dk. Bashiru amesema, ni kiongozi mzuri na kwamba, kuna baadhi ya maeneo anahitaji kupikwa.

Nape ambaye aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa Itikadi na Uenezi wa CCM pia Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ametajwa na Dk. Bashiri kwamba ni jasiri.

Dk. Bashiri alitoa kauli hiyo baada ya kuulizwa na mtangazaji maoni yake kuhusu misimamo ya wabunge wa CCM ambao wamenukuliwa wakitoa kauli kali kwa serikali iliyoko madarakani.

“Nape ni mwenezi wetu, jasiri kabisa lakini anahitaji kupikwa,” amesema Dk. Bashiri akiongeza “nilichokuwa nasema siyo nakubali kila kitu, bali mtambue kuwa, chama kina wajibu wa kuwasikiliza, kuwaandaa, kuwaamini na kuwasimamia kama wanakwenda inavyotakiwa.”

Dk. Bashiru amesema, kutokana na mazingira ya sasa yalivyo, Nape na Bashe ni kati ya watu ambao wana mchango mkubwa.

Amesema, kutokana na umuhimu wa kuandaa vijana, wameomba kijengwe chuo cha kuandaa viongozi kutoka nchi sita tofauti.

“Lengo ni kuandaa viongozi waliochipukia kwa sababu suala hili linahitaji maarifa na bila shaka tutakuwa na kina Nape na Bashe wengi,” amesema Dk Bashiru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mikataba ya utekelezaji bado haijasainiwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

error: Content is protected !!