Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Bashiru: Msiombe JPM adumu madarakani
Habari za Siasa

Dk. Bashiru: Msiombe JPM adumu madarakani

Spread the love

FIKRA kwamba, Rais John Magufuli anapaswa kuendelea kuwepo madarakani hata baada ya kumaliza muhula wake wa pili iwapo atachaguliwa, wametakiwa kuzika fikra hizo. Anaripoti Danson Kaijage…(endelea).

Dk. Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM amewataka makada wa chama hicho kutoomba dua hiyo na kuwa, ameshauri kuimarisha chama chao ili kiendelee kutoa viongozi bora.

Akizungumza katika Uzinduzi wa Mkakati Maalum wa CCM wa kukomaza demokrasia nchini uliofanyika jijini Dodoma, Dk. Bashiru amesema, chama hicho kina kazi ya kuhakikisha kinatoa viongozi bora kama Rais Magufuli, na si kubadili utaratibu na kuomba kiongozi huyo kuongoza muda mrefu.

Amesema, CCM ina mbegu za kuzalisha viongozi bora na kuwatoa wasiwasi baadhi ya watu wanaofikiria hatma ya Tanzania baada ya Rais Magufuli kumaliza uongozi wake.

“Naomba kuhitimisha mjadala usio rasmi, unaoendelea kuhusu hatma ya nchi hii baada ya Dk. John Pombe Magufuli. Hatma ya nchi hii iko mikononi mwa wana-CCM.

“CCM inahazina ya viongozi bora wakati wote wanaCCM na hasa wakina mama wana CCM wanambegu bora za kuzalisha viongozi wa kutosha,” amesema Dk. Bashiru na kuongeza;

“Kwa hiyo kazi ya kutuhakikishia kuwa na viongozi bora kama Dk.  Magufuli si kuomba dua ya kukaa muda mrefu madarakani au kubadilisha taratibu tulizonazo, bali ni kuimarisha chama chetu, kwa hiyo mkakati huu unalenga kutukumbusha kwamba CCM ina hazina ya viongozi bora.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!