Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Bashiru: CCM itaongoza zaidi ya miaka 100 ijayo
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Bashiru: CCM itaongoza zaidi ya miaka 100 ijayo

Dk. Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM
Spread the love

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ally amesema kuwa, chama hicho kitaendelea kuongoza dola kwa zaidi ya miaka 100 ijayo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza kwenye ziara yake mkoani Mwanza leo tarehe 22 Mei 2019, katibu huyo amesema, CCM ina misingi iliyo imara inayokiwezesha kuendelea kuwepo madarakani.

Dk. Bashiru yupo ziarani Mwanza kukagua miradi ya CCM ambapo amesema, chama hicho hakiwezi kuondolewa madarakani kwa kuchagizwa na mijadala ya mitandaoni.

“Kuiondoa CCM madarakani kunahitaji kuwa na mkia mrefu,” amesema Dk. Bashiru akisisitiza kuwa, kura zinapigwa na wananchi na sio mitandaoni.

Dk. Bashiru amesema kuwa, fikra sahihi kwa wanachama, uhuru na usawa ndio nguzo muhimu inayokiwezesha chama hicho kuendelea kuwa na ndoto ya kutawala dola kwa zaidi ya miaka 100 ijayo.

 “Serikali ambayo inahakikisha inalinda rasilimali, haipangiwi cha kufanya, kulinda uhuru sambamba na kuwekeza kwa wananchi, itakuwepo kwa muda mrefu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!