KAULI iliyowahi kutolewa na Humphry Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM visiwani Zanzibar mwaka jana kwamba, kambi hazitasidia kupata mgombea, leo tarehe 3 Novemba 2019, imetolewa na Dk. Bashiru Ally. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Akiwa Pemba, Dk. Bashiru amezungumza kwenye kamati ya siasa Wilaya ya Chakechake, kwamba mikakati yao ya kutaka kupitishwa ili kugombea udiwani, ubunge na hata urais, inakiuka miiko ya chama hicho.
Dk. Bashiru yupo ziarani visiwani humo, ambapo amekuwa akikutana na viongozi mbalimbali pamoja na wanachama wa chama hicho.
Akizungumza Chadekchake Dk. Bashiru amesema, tayari ana taarifa kuhusu kuwepo kwa hekaheka za baadhi ya wanachama wao wakilenga kuteuliwa kugombea nafasi mbalimbali.
Mwaka jana, akiwa ziarani Zanzibar, Poleple aliwaonya wanachama wa visiwa hivyo kwamba, wanaojipitisha na kupanga mikakati ya kumrithi Dk. Mohammed Shein, rais wa sasa visiwani humo, wanajihangaisha.
Alisema, hakuna anayemfahamu mrithi wa Dk. Shein na wasidhani atapatikana kwa utaratibu waliouzoea. “Mimi niwaambie msijisumbue! chama kitamtoa “mtu wake” Dodoma; mtaletewa mumpigie kura huyo.”
Leave a comment