Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Diwani, dereva wa Halmashauri Meatu wafariki ajalini
Habari za SiasaTangulizi

Diwani, dereva wa Halmashauri Meatu wafariki ajalini

Spread the love

DIWANI wa Kata ya Manuzi, Elias Shukia na dereva wa halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Haruna Ngata wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka mkoani Dodoma, kupasuka tairi na kupinduka mara tatu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa za awali kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Miraji Mtaturu zinaelea kuwa ajali hiyo imetokea eneo la Mkiwa, Wilayani Singida.

Mtaturu amesema mkuregenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Fabian Manuzi; mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Piuz Machungwa na watu wengine wanne wamejeruhiwa katika ajali hiyo.

Amesema majeruhi wanne wamelazwa katika hospitali ya St Gasper iliyopo Itigi na wawili wamelazwa hospitali ya Puma iliyopo wilayani Ikungi.

“Chanzo tulichokiona kwenye eneo la tukio ni kupasuka kwa tairi la mbele kushoto, hata hivyo tuwasubiri polisi wafanye uchunguzi zaidi watatuambia chanzo cha ajali yenyewe,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!