KATIKA muendelezo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma, Mariam Ditopile (CCM) ameungana na Waumini zaidi ya 500 katika Msikiti mkubwa Kata ya Mkoka, Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma katika Iftari na Dua Maalum ya kuiombea Nchi na kumuombea Rais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Kabla ya dua hiyo Mbunge alitembelea Shule ya Msingi Mkoka Kitengo Maalum cha Wanafunzi wenye mahitaji Maalumu (walemavu) na kuwapelekea sadaka, vitabu, kalamu na mahitaji ya shule mbalimbali.
Mbunge hiyo Viti Maalum Mkoa wa Dodoma, anaendelea kuwatakia Waislamu wote nchini Ramadhani njema.
Leave a comment