Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko DIT inavyojipanga kukabili soko la ajira
Habari Mchanganyiko

DIT inavyojipanga kukabili soko la ajira

Spread the love

TAASISI ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) inakusudia kuboresha mitaala ya shahada mbili za umahiri (masters) ili kuendana na ushindani wa soko la ajira ndani na nje. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Pia, lengo la maboresho hayo ni kuwawezesha wahitimu kuwa na uwezo mkubwa ikiwemo kujiajiri.

Jana Jumanne tarehe 11 Agosti 2020, DIT ilikutana na wadau mbalimbali ili kujadiliana jinsi ya kuboresha mitaala hiyo.

Shahada zinazoboreshwa ni Master of Computational Science and Engineering-MCSE na Master of Maintenance in Engineering and Management-MENG).

Mkuu wa Idara ya Masomo ya Umahiri, Utafiti na Machapisho wa DIT, Profesa Leonia Henry, anasema kuwa wataangalia eneo la ufundishaji, vifaa vinavyotumika kufundishia na maendeleo ya kidijitali.

“Mchakato huu ukikamilika, mitaala iliyoboreshwa itaanza kutumika katika mwaka mpya wa masomo unaonza Novemba 2020,” alisema Profesa Leonia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

error: Content is protected !!