Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Dirisha maombi ya kujiunga vyuo vikuu kufunguliwa Julai 15
Elimu

Dirisha maombi ya kujiunga vyuo vikuu kufunguliwa Julai 15

Katibu Mtendaji TCU, Charles Kihampa
Spread the love

TUME ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imetangaza kwamba, maombi ya kujiunga na vyuo vikuu kwa shahada ya kwanza katika mwaka wa masomo wa 2019/20, yataanza rasmi tarehe 15 Julai 2019. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 13 Julai 2019 na Profesa Charles Kihampa, Katibu Mtendaji TCU.

Prof. Kihampa amewataka wenye sifa za kudahiliwa kusoma kwa makini, vigezo vilivyo orodheshwa katika kitabu cha muongozo wa program zilizoanishwa na TCU, wathibitishe kama wana sifa stahiki za udahili zilizoainishwa na tume hiyo.

Pia, Prof. Kihampa amewataka waombaji wenye vyeti vilivyotolewa nje ya nchi kuviwasilisha vyeti vyao Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) au Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), ili kupata ithibati ya ulinganifu wa sifa zao kabla ya kuanza kuomba udahili.

Aidha, Prof. Kihampa amewataka wananchi kuwa makini na watu wanaojiita mawakala au washauri wa namna ya kujiunga na vyuo vya elimu ya juu hapa nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!